Welcome to
Tanzania

Kanisa la Kikristo Tanzania

Mfuate Yesu anayetufundisha kumpenda Mungu, kumpenda kila mtu, kufanya wanafunzi, na kusimulia habari zetu.

Injili zinaelezea ujumbe wa Yesu: Alienda mji hadi mji akitangaza toba na kuja kwa ufalme wa Mungu.
Na kila mtu aliyekutana naye, amri ya kwanza aliyoitoa Yesu ilikuwa rahisi:

Nifuate.

Hii bado ni amri tunayoisikia wakati tunapoyatoa maisha yetu kwa kumwamini Kristo, hivyo amri hii ni ujumbe wa Kanisa la Kikristo Tanzania. Tupo kwa ajili ya kumfuata Yesu. Jina la mwanzo la mwenendo wa Kikristo lilikuwa “Njia” kwa sababu walifuata njia ya Yesu, na tunatafuta kuishi katika mwendelezo wa mwenendo wa mwanzo.
Kama wafuasi tunafungamanishwa na amri muhimu za Yesu: Amri Kuu (Marko 12:28-31) na Maagizo Makuu (Mathayo 28:18-21 na Matendo ya Mitume 1:8). Kiini cha amri hizi ndizo zinazoongoza kila tunachokifanya katika Kanisa la Kikristo Tanzania.
Kwa hiyo, sisi kama wafuasi wa Yesu:

Mpende Mungu

hivyo tunaishi kama wanaoabudu

Mpende kila mtu

hivyo tunaishi kama watumishi

Kufanya wafuasi

hivyo tunaishi kama wafuasi

Kusimulia habari zetu

hivyo tunaishi kama Wamisionari

Hizi amri nne ni alama za maisha yetu ya pamoja kama wafuasi au wanafunzi wa Yesu. Tunatambua kwamba hatumfuati Yesu isipokuwa tuwe watii kwa hizi amri zake kama zilivyoelezwa katika utume wetu wa pamoja na maisha yetu binafsi. Kila programu, utendaji, na mpango katika Kanisa la Kikristo Tanzania unaongozwa na ujumbe huu, na kila mshirika wa Kanisa la Kikristo Tanzania ana changamoto ya kufungamanishwa na ujumbe huu katika maisha yao.

Tunachoamini

Mwanzo 1; Yohana 3:16

Mungu Mmoja

Kuna Mungu mmoja aliyeumba vitu vyote na anavipenda vitu vyote. Mungu anakupenda hasa wewe. Mungu alikuumba kwa makusudi na kwa lengo. Mungu ni wa milele na msukumo wake ni wa upendo wa milele kwa ulimwengu wote unaomhusisha kila mmoja nawe ukiwemo.
2 Timotheo 3:16,17

Biblia

Biblia ndiyo kanuni yetu pekee ya kile tunachokiamini na kile tunakichofanya. Tunaamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu na ina mamlaka na yenye kutegemewa katika yote inayofundisha. Ni mwangaza wa Mungu na ni muhimu kwa kutufundisha jinsi ya kuishi na kujifunza katika haki ambayo Mungu anatamani kwa maisha yetu.

Yesu

Yesu ni Mwana wa Mungu aliye hai. Yeye ndiye mfalme aliyepakwa mafuta (Masihi au Kristo) aliyeahidiwa na manabii wa Agano la Kale. Alichukua mwili na kuishi katika historia ili awaite wanafunzi, atufundishe namna ya kuishi, na hatimaye kufa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu wote, na kufufuka kutoka kwa wafu baada ya siku tatu. Sadaka yake humaanisha kwamba dhambi zetu zinaweza kusamehewa, na tunaweza kuunganishwa tena na Mungu aliyetuumba na anayetupenda. Ufufuko wake huonyesha kwamba kifo kimeshindwa, na kwamba wote wamwaminio Kristo wataishi milele pamoja na Mungu.
Tunaamini kwamba Yesu atakuja ili akamilishe kazi ya utawala wa Mungu na kuishi milele pamoja na watu wa Mungu katika dunia mpya ya milele.

Roho wa Mungu

Roho Mtakatifu anaishi ndani ya wale wanaomwamini Yesu Kristo kama Mfariji na Mtetezi na kutusaidia zaidi kuwa kama Yesu kupitia mawazo, maneno, matendo, na tabia.
Agano Jipya linatufundisha utume wa wote wanaoamini, kwa kutambua kuwa Roho Mtakatifu hutoa karama mbalimbali kwa waamini wa kanisa kusudi kila mshirika au muumini aweze kutoa mchango wenye matokeo kwa kanisa lote.

Kwa hiyo, sisi ni kanisa lililojaa Roho katika kuyafanya mapenzi ya Mungu na kuwa zaidi kama Mwana wa Mungu, Yesu Kristo. 

1 Wakorintho 12:12-27

Kanisa

Kanisa ni mwili wa Kristo duniani, na ni mpango wa Mungu wa kuufikia ulimwengu. Tumepewa jukumu la kuendeleza utume au ujumbe wa Kristo wa kutangaza habari njema, na kuuishi ufalme wa Mungu hadi Kristo atakaporudi. Kanisa limejazwa na watu wasio wakamilifu ambao wanapendwa sana na Mungu, na wanaopendana kwa kusudi la kuendeleza utume au ujumbe wa Mungu.
Maamuzi yote ya uongozi hufanywa na wazee ambao huchaguliwa na kusanyiko na ambao wamepewa jukumu la uongozi wa kiroho na wa vitendo wa kanisa. Kwa pamoja, tunashiriki umoja katika Bwana mmoja, imani moja, na ubatizo mmoja. Tunashiriki mwaliko wa Yesu kwa komunyo kwa wote wanaoamini. Tunafanya hivi pamoja kama washirika wa kanisa hili wanaofuata amri kuu za Kristo na kutaka kutimiza maagizo makuu.
Ingawa ushirika hauhitajiki ili kushiriki katika Kanisa la Kikristo Tanzania, tunawaalika wale wanaotaka kushirikiana nasi katika huduma kuwa sehemu ya kanisa. Tunahitaji ushirika ulio katika maandiko: Kukiri hadharani kwa imani katika Kristo kama mwokozi na Bwana, na ubatizo wa kuzamishwa kama kielelezo cha imani hiyo na ishara ya kifo cha Kristo, kuzikwa na ufufuko.
Warumi 3:21-24; Waefeso 2:8-10

Wewe

Neno la Mungu linafundisha kwamba watu wote wameumbwa kwa mfano wa sura ya Mungu, ijapokuwa sura hiyo imeharibiwa ndani yetu, bado Mungu anakusudia mambo mema kwenye maisha yako. Wewe ni tunu ya Mungu na umejaliwa na Mungu kufanya kazi ambayo Mungu amekuandalia. Moja ya mambo bora tunayotakiwa kufanya maishani ni kutambua kazi gani nzuri tuliyoandaliwa na Mungu kwenda kuifanya.
Matendo ya Mitume 4:8-12; Waefeso 2:8-9; Yohana 3:16-18; Matendo ya Mitume 8:26-38; Warumi 6:1-4

Wokovu

Watu wote wanahitaji kazi ya uokozi wa Mungu katika maisha yao. Mungu anataka kukusamehe dhambi zako na kukuponya majeraha yako. Mungu anataka akufanye uwe kiumbe mpya na kukuweka uwe katika familia ya Mungu. Wokovu huu unawezekana kwa sababu ya neema ya Mungu isiyo na kikomo kwako. Si jambo ambalo mtu yeyote hutimiza kwa kuishi maisha mazuri au kwa kwenda kanisani. Ni zawadi kutoka kwa Mungu inayopokelewa kwa kumwamini Kristo kama Bwana na Mwokozi. Biblia inatufundisha kwamba tunaweka alama ya imani hii kwa kubatizwa kama kielelezo cha imani yetu.

Email:

philipbuluba@gmail.com

Address:

PO Box 84 Bunda Tanzania

Phone:

+255 756 858 793

© 2023 Tanzania Christian Church. All Rights Reserved.